Changamoto za Corona

Covid

Vilio huku na huku, kila mmoja ni Korona

Nyoyo mejawa shauri,wanadamu twasonona

Tunakufa kama kuku, uchumi kwama kina

Waziona atharizo? Watutesa sema mbona

 

Dada zetu taabani, kisa korona nyanjani

Mimba Tele hesabuni, visa vipya kupandani

Vidume ni wani wani, kisawe wadanganywani

Waziona atharizo? Watutesa sema mbona

 

Wenda pasi ufahamu, wa njia zilo salama

Ila swezi walimu, mana Hawaii njema

Kupityawe wadhulumu, ona yanowaandama

Waziona atharizo? watutesa sema mbona

 

Serikali mashakani, wakumnusuru nani?

Usalama mipakani? Ama vijana nyumbani?

Wagonjwa sipitalini, ama wewe maluuni?

Waziona atharizo? watutesa sema mbona

 

Tamati tama sikatai, ingawa wajona bingwa

Sanitaza kwa wakati, naamini utashindwa

Barakoa ni shuruti, umbali ulishapangwa

Waziona atharizo? Watutesa sema mbona

Chairman, Mombasa County, Teddy Ruwa

2 thoughts on “Changamoto za Corona”

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Posts

Shopping Cart